Mariolojia ya Kikatoliki

Ukuu wa Bikira Maria unamtegemea Mwanae, Yesu.
Stabat Mater, yaani picha ya Bikira Maria chini ya msalaba wa Yesu, kadiri ya Gentile wa Fabriano, 1410-1412 hivi.

Mariolojia ya Kikatoliki inategemea Biblia ya Kikristo pamoja na Mapokeo ya Mitume yanayojitokeza hasa katika maandishi ya Mababu wa Kanisa wa Mashariki na wa Magharibi. Hayo yote yaliongoza Mapapa na maaskofu wenzao wa Kanisa Katoliki kutangaza hasa dogma nne kuhusu Bikira Maria.

Mafundisho makuu hayo ni lazima kila Mkatoliki ayasadiki kutokana na ufunuo wa Mungu:

  1. B. Maria mkingiwa dhambi ya asili
  2. B. Maria Mama wa Mungu
  3. B. Maria Bikira daima
  4. B. Maria kupalizwa mbinguni mwili na roho

© MMXXIII Rich X Search. We shall prevail. All rights reserved. Rich X Search